
Bogumil Jewsiewicki Koss
Università Laval, Québec, Canada
Novembre 2012
Kukusanya haya matableaux ya peinture ya mu cité kulifanika kati ya mwaka 1968 na 2005. Nilinunua tableau ya kwanza katika hoteli moja mjini Boende, na kisha nilipata yale ya Mbandaka na Kinshasa. Kwa hivi, nilijiwekea shabaa ya kukusanya documentation juu ya namna watu wanacréaka vitu mu mavilles ya leo. Ile miaka wengi walianza kufikiri asema ukoloni uliuwa créativité kati ya watu wa Afrika ya kati. Kwa waautorités wa Zaïre inye ilionekana kuwa na faida ni maoeuvres d’art ya mbele ya ukoloni, yakionyesha technicité (ya ule wakati) na maoeuvres d’art ya kizungu (moderne) yalitokea ku masomo ya Beaux-Arts. Bila shaka, sikuwa peke yangu: Victor Bol na Joseph Cornet, Johannes Fabian na Ilona Szombati nao pia walipenda maoeuvres d’art plastique ya mu ville.
Shabaa yangu ya pili ilikuwa ni kutambua jinsi kuona kwa watu kunaenda mu kubadilika wakati wanasimulia historia ya inchi yao kupitia art plastique (yenye kuumbwa na mikono ya watu: tableaux , kuchonga sanamu….), habari za maisha na muziki. Kufika kwangu mjini Lubumbashi mu 1971 na safari kwa ajili ya utafiti katika jimbo la Katanga, Kivu na Province Orientale vilinipa maoccasions mengi ya mimi kuweza kukutana na wapeintres wengi na tena kununua matableaux mengine mapya. Kama vile Johannes Fabian ku mwanzo wa maannées 70, nilikuwa nikionana na Tshibumba Kanda Matulu na nilinunua matableaux yake mengi. Mu maannées 80,sikua tena naishi mu Kongo, lakini nilikuwa nikirudi kule mara mingi; warafiki wengine nao walinisaidia kupata matableaux mengine. Kazi ya watafiti wengine Wakongomani na Projet ya Ukumbusho wa Lubumbashi, inye ilianzishwa mu 2000 juu watu wasisahabu mambo yalipitakana mu mavilles, vilitufungulia njia za sasa. Mu Lubumbashi, akiongozwa na Donatien Dibwe dia Mwembu, Michel Ange Ntambwe Banze, alitumika juu ya wapeintres
na alinunua mamia ya matableaux , mpaka alipofariki dunia mwaka 2001. Jean-Pierre Nzunguba Ibio alifanya thèse yake ya doctorat juu ya wapeintres mu Bunia naye vilevile akanunua mamia ya matableaux. Biaya Tshikala, aliyefariki mu 2002, alifanya utafiti wake mu Kongo ku Kasai na Kisangani, lakini Mwewa Kasongo aliendesha utafiti wake mjini Lubumbashi juu ya uzuri (urembo) wa matableaux ya wapeintres wa mu jimbo la Katanga na kuona jinsi watu wako wanayapokelea.
Ku mwanzo wa maannées 90, jimbo la Katanga lilitatizwa na crise économique pamoja na kufukuzwa kwa watu kikabila: watu wengi wakaanza uzisha mali yao yote, ata na matableaux . Wakati ule Léon Verbeek na mimi mwenyewe tulinunua zaidi ya matableaux tukisaidiwa na wainformateurs wetu. Yale matableaux yanashuudia kufanywa na kupokewa na wakaaji kwa matableaux ya maannées 70 na 80.
Katika miaka kumi iliyofuata, mkusanyo wangu ulizidi kuongezeka. Wakati ule ule mkusanyo mwingine ulianzishwa katika Projet ya Ukumbusho wa Lubumbashi na Léon Verbeek, naye, akaanza kukusanya matableaux yake.Musée ya art africain ya New York ilitengeneza exposition ya matableaux juu ya maisha na kifo cha Patrice Émery Lumumba. Wakati mojamoja ule, mimi kwa upande wangu niliendelea kununua matableaux mjini Kinshasa na, pamoja na Barbara Plankensteiner, nilitengeneza exposition juu ya matableaux ya mavilles ya mu Kongo ku Musée ya Volkerkunde mjini Vienne. Mwaka 2011, tukiungana mkono na Université ya Calabria, tulitengeneza pale Roma na Cosenza, exposition juu ya “Urithi wa Lumumba. Uhuru wa Kongo katika matableaux ya mu cité”(mijini Cosenza na Roma).
Juu ya Katanga, ku wale wanaotaka kufahamu mengi, wanaweza pia kutazama mkusanyo wa Léon Verbeek ku site web ifwatayo (http://lubumarts.africamuseum.be) na vile vile wanakaribishwa ku site web ya Johannes Fabian kuhusu culture ya cité ya Afrika ya kati (http://lpca.socsci.uva.nl).